×

Lissu Ataka Kukutana na IGP Wambura, CDF Mkunda na Kingai Kupanga Mkakati wa Ushahdi Wa Kesi

Mhe. Tundu Lissu ameieleza Mahakama kuwa John Heche ndiye shahidi wake wa mwisho ambaye ni raia, akisema anaamini re-examination yake itakamilika kesho kwa muda usiozidi saa moja.

Aidha, Lissu aliomba mashahidi wake wengine waliobaki wafike ili aweze kukutana nao na kupanga namna ya kuendelea na ushahidi uliosalia ambapo kauli hiyo ilizua vicheko ndani ya ukumbi wa Mahakama baada ya kutoa hoja hiyo.

Awali, Jaji Ndunguru alimweleza Lissu kuwa bado ana mashahidi watatu na kwamba Mahakama ilitarajia upande wa utetezi kuwasilisha final submissions siku ya Ijumaa.

Hata hivyo, Lissu alieleza kuwa anahitaji kwanza kukutana na mashahidi hao ili kupanga mkakati wa kesi.

Mashahidi hao ni IGP Camillius Wambura, Mkuu wa Jeshi la Polisi Tanzania; CDF Jenerali Jacob John Mkunda, Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi ya Wananchi wa Tanzania; pamoja na DCI Ramadhan Kingai, Mkuu wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai.

Baada ya maelezo hayo, Jaji Ndunguru aliahirisha shauri hadi kesho saa tatu kamili asubuhi, huku akibainisha kuwa shahidi John Heche bado hajamaliza kutoa ushahidi wake.

Leave a Comment