×

Kijana Awashambulia Abiria Kwenye Treni Ujerumani

3665566A00000578-3696410-image-a-32_1468884757572

KIJANA mmoja aliyekuwa na kisu na shoka amewashambulia abiria waliokuwa kwenye treni huko Kusini mwa nchi ya Ujerumani jana usiku na kuwajeruhi watu wanne.

Kijana huyo baadaye alipigwa risasi na Polisi na kufa alipokuwa akikimbia baada ya tukio hilo.

160718220643_german_train_axe_attack_640x360_epa_nocredit

Polisi wa mjini Wuerzburg wameeleza kwenye ukurasa wao wa Facebook kuwa abiria watatu wamejeruhiwa vibaya na wengine 14 wanapata msaada wa kitabibu kutokana na mshtuko walioupata.

Polisi wamesema bado hakuna taarifa yeyote kuhusu sababu ya kutekelezwa kwa shambulio hilo.

3665122500000578-3696410-image-a-1_1468876428027

vyombo vya habari vya Ujerumani vimemnukuu msemaji wa wizara ya mambo ya ndani mjini Bavaria kuwa mtu huyo ni mvulana wa miaka 17, mkimbizi mwenye asili ya Afghanistan.

3665124100000578-3696410-image-m-12_1468876685588

Kabla ya kushambulia treni, kijana huyo alisikika akiongea kwa sauti ‘Allahu Akbar’ na uchunguzi uliofanywa umebaini bendera iliyochorwa kwa mkono kwenye chumba chake.

36654D4900000578-3696410-image-a-25_1468881849632

Leave a Comment