The House of Favourite Newspapers

Shoga:Usisahau choroko nazo mboga

0

chorokoKILA inapofika siku ya leo Jumanne nikiwa mzima wa afya huwa namshukuru Mungu, natumai na wewe hufanya hivyo.

Wiki iliyopita nilizungumzia kuhusu tui la nazi lazima lionjwe. Lazima liandaliwe kwa chakula cha usiku shoga, hupendwa na wananaume wa shoka, tui zuri lile la kwanza siyo la pili, linakuwa laini na tamu, mwanamke sharti ujue jinsi ya kulitumia katika chakula, upo?

Baada ya hayo tuelekee kwenye mada yetu ya leo ambayo imenishangaza na hapa nilipo niwachane wale mashoga zangu wanaosahau choroko nayo ni mboga na inatakiwa kuliwa katika chakula cha usiku.

Shoga, ili uitwe mwanamke wa Kiafrika lazima ujue mapishi ya choroko, ujue rangi za choroko na kuzipamba kabla hamjala chakula cha usiku haijalishi mnakula na ugali ama wali.

Wanaume wengi wa kimjinimjini siku hizi wanakata tamaa ya kula chakula cha usiku na mtu wake wa muda mrefu kwa sababu tu hakuna choroko, embu fikiria mnakuwa pamoja mezani ama ukumbini kila mwenzako akitafuta choroko hazioni, shtuka shoga, utaachwa looh!

Wengine wanaona ni kama wamepikiwa chakula na mwanaume mwenzake kwani hakina ladha kwa kukosa choroko. Wanaona bora hata picha za mitandaoni zilizopambwa kwa choroko zina mvuto!

Shoga kikubwa tuache usasa, uzuri wa mwanamke kutosahau kama choroko nayo ni mboga, lazima ifunuliwe na mwanaume na kuliwa. Kama unashindwa kutengeneza choroko nyingi basi tafuta choroko chache zitumie kwenye chakula na mumeo.

Mashoga zangu wengine wanaona kuandaa choroko kwa ajili ya chakula cha usiku ni jambo lililopitwa na wakati, wamebaki kung’ang’ana kuandaa chakula wakiwa na micheni ya silva na dhahabu kila kona, jamani huo utamaduni wa wenzetu!

Ngoja nikumegee shoga maana mi na wewe tena! Shuuu! Choroko ni moja ya mboga zinazopendwa na wanaume hasa katika chakula cha usiku. Asilimia kubwa ya wanaume wakimuona mwanamke yeyote akijiachia na choroko kwenye ungo amezianika waziwazi iwe barabarani, kwenye daladala lazima atamani, upo?

Shoga, choroko inaleta utamu katika chakula. We huoni raha iliyoje unapomfunulia chakula mumeo kisha anakutana na choroko zikiwa zimepambwa kwa mistari ya kuvutia kwa rangi, ushafikiria ukiziunga na karoti je, zinakuwaje? Acha kabisa shoga!

Wanaume wa zamani walikuwa wanapenda kabla hawajala tu chakula cha usiku, wanazivamia choroko na kuanza kuchagua mojamoja tena wengine wanazifumbia macho kwa jinsi zilivyo tamu na kuanza kuzila kwa kuzipapasa kwa maana ni tamu, usiombe shoga! Atakuachaje kwa mfano?

Shoga nikuulize tu, najua mazumbukuku mjini wapo, usikute hata na wewe unampikiaga tu mumeo au ulishaacha lakini hujui kama choroko zina rangi zake na kila choroko ina maana yake.

Mfano ukimuunguzia mumeo choroko zikawa kama nyekundu ina maana hamtakiwi kula chakula cha usiku siku hiyo, upo? Zisipoiva sana zikawa nyeupe maana yake mnaweza kula chakula cha usiku bila wasiwasi na kama sasa umeziunguza na kuwa nyeusi kama chungu basi jua usiku huo zitaliwa kishida kwa maana chakula kitakuwa kimejaa na ukoko mwingi, asalalee!

Ndiyo maana wanaume wa zamani shoga walikuwa wanajua kuwasiliana na wake zao kabla hawajarudi majumbani ama wakirudi kabla ya kuvamia meza na kula chakula cha usiku wakikutana na choroko za rangi hizo anajua ale ama asile.

Binti wa Miaka 19 Aliye Tembea na Wake za Watu Ndiye Huyu Hapa-Part I

PT 2- Binti wa Miaka 19 Aliye Tembea na Wake za Watu Ndiye Huyu Hapa-Part I

Mzungu Dar Afumwa Live Akilawitiwa na Vijana 3, O.F.M Yanyaka Tukio Zima

Leave A Reply