Waliokuwa wafanyakazi wa Kampuni ya Optima Aviation wakiwa nje ya Ofisi za NSSF Posta jijini Dar.
Wakiendelea kusimama nje ya ofisi hizo.
Baadhi ya askari wakijaribu kuwatuliza.
Baadhi ya wanahabari wakichukua maoni yao.
Mmoja wa wafanyakazi hao aliyejitambulisha kwa jina la Gaspar Mpanda, akihojiwa na Global TV.
Kundi la waliokuwa wafanyakazi wa Kampuni ya Ulinzi ya Optima Aviation limevamia ofisi za Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) zilizoko Ilala na Posta leo jijini Dar es Salaam wakitaka mafao yao baada ya kuacha kazi. Wafanyakazi hao wanadai kero ya kudai mafao yao ni ya muda mrefu ndiyo maana wameamua kwenda kwenye ofisi hizo.
NSSF wameeleza kuwa kampuni hiyo haijawasilisha makato ya zaidi ya shilingi milioni 100 katika mfuko huo.




