×

Kocha Mkenya Atimuliwa Olimpiki Rio Brazil

KENYA OLYMPIC (2)Kocha wa timu ya riadha ya Kenya inayoshiriki michuano ya Olimpiki mjini Rio de Janeiro amerudishwa nyumbani kwa kosa la udanganyifu.

KENYA OLYMPIC (1)Ferguson Rotich.

Mkuu wa Timu ya Olimpiki ya kenya, Kip Keino amesema John Anzrah aliigiza kama miongoni wa wakimbiaji wa mita 800, na kutoa sampuli ya mkojo kwa niaba ya mwanariadha Ferguson Rotich.

KENYA OLYMPIC (5)Kip Keino

Udanganyifu uligundulika na wakaguzi wa dawa za kusisimua misuli baada ya kuangalia picha za kitambulisho alichokuwa amevaa, ndipo walipogundua kuwa sura ya Bw Anzrah haeindani na mchezaji aliyefanya uchunguzi.

KENYA OLYMPIC (3)Rais wa Kenya, Uhuru Kenyatta na wanariadha wa nchi hiyo.

Mkuu wa Timu ya Olimpiki ya Kenya, Kipchoge Keino amesema uongozi wa timu yake hautavumilia tabia hiyo ingawa mpaka sasa hakuna hatua yoyote iliyotolewa dhidi ya Rotich.

KENYA OLYMPIC (4)Michael Rotich

Anzrah ni afisa wa pili kutoka kenya kurejeshwa nyumbani, wa kwanza akirudishwa kwa kosa la kuomba rushwa ili kuweza kukwepa upimaji wa matumizi ya dawa za kusisimua misuli.

KENYA OLYMPIC (6)Wanariadha wa Kenya Collins Injera, David Rudisha, Julius Yego na Humphrey Kayange.

Kumekuwa na idadi kadhaa ya wanariadha wa Kenya ambao walishindwa kufuzu vipimo vya matumizi ya dawa za kuongeza nguvu huku ni wiki iliyopita tu shirika la kupambana na matumizi ya dawa hizo WADA likiiondoa Kenya kwenye nchi zilizoshindwa kutimiza masharti.

Leave a Comment