The House of Favourite Newspapers

MH! SHEMEJI YETU KWA WOLPER KULIKONI?

0

KAPO mpya inayotikisa kwa sasa Bongo ni ya muigizaji Jackline Wolper na baby wake, mwanamitindo anayeitwa Brown.
Tangu kuibuka kwa kapo hiyo ambayo wote wawili wanaonekana kuzama kwenye dimbwi zito la mahaba, kumekuwa na tetesi nyingi zinazomhusu shemeji yetu huyo ikiwemo ile ya kuwa ni mume wa mtu ambapo kwa nguvu zote amekanusha taarifa hizo.


Yote tisa, kumi ni hii hapa! Inadaiwa kuwa eti… mwanamitindo huyo amewahi kujihusisha na mapenzi ya jinsia moja na hili limeibuka baada ya kusambaa kwa picha mitandaoni inayomuonesha shemela akiwa katika pozi kitandani na mwanaume mwenzake.
Ebwana dah! Unaambiwa mitandao ya kijamii imechafuka baada ya kuzagaa kwa picha hiyo, kila mmoja anasema lake lakini je, ni kweli? Mimi na wewe hatujui, tuendelee kusubiri maelezo kutoka kwa mhusika.
Na Isri Mohamed, GPL.

Leave A Reply