SHINDA NYUMBA YAACHA GUMZO MKURANGA
Kuelekea droo kubwa ya Bahati Nasibu la Shinda Nyumba Awamu ya Pili kutoka Kampuni ya Global Publishers, wachapichashaji wa magazeti ya Champion, Uwazi, Ijumaa, Ijumaa Wikienda, Amani, na Uwazi, promosheni ya shindano hilo mwishoni mwa wiki hii imeacha gumzo wilayani Mkuranga mkoani Pwani.
Gumzo hilo limeachwa na timu nzima ya masoko kutoka Global Publishers wakiongozwa na Mr Shinda Nyumba punde baada ya kuwasili wilayani humo. Utitiri wa watu walikusanyika kushuhudia urefu wa Mr Shinda Nyumba huku wakinunua magazeti ya Global na kujaza kuponi sanjari na kupiga picha na Mr Shinda Nyumba.
Ofisa Masoko wa Global Publishers, Jimmy Haroob, alipata nafasi ya kuzungumza na wakazi wa Mkuranga na kuwaasa kuendelea kuchangamkia ujazaji wa kuponi kwa kununua magazeti ya Global Publishers katika siku hizi za mwishomwisho kuelekea kilele cha shindano hilo ambapo mshindi atajinyakulia nyumba ya kisasa iliyojengwa kwa mamilioni ya shilingi. Nyumba hii, inapatikana Bunju jijini Dar es Salaam.
[…] wakati walipotembelewa na timu ya promosheni ya Shinda Nyumba, wakazi hao ambao ni wasomaji wa magazeti yanayochapishwa na Global Publishers ambayo ni Ijumaa, […]