The House of Favourite Newspapers

TAARIFA MUHIMU KUTOKA IKULU

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli tarehe 10 Desemba, 2018 amepokea hati za utambulisho za Mabalozi 2 kutoka nchi za Ethiopia na Misri walioteuliwa kuziwakilisha nchi hizo hapa nchini.

 

Mabalozi waliowasilisha hati zao ni Mhe. Yonas Yosef Sanbe – Balozi wa Ethiopia hapa nchini na Mhe. Mohamed Gaber Mohamed Abulwafa – Balozi wa Misri hapa nchini.

 

Mabalozi hao wamemshukuru Mhe. Rais Magufuli kwa kuwakaribisha hapa nchini na wameahidi kuwa katika kipindi cha uwakilishi wao watahakikisha wanaimarisha na kukuza zaidi uhusiano na ushirikiano wa nchi hizo na Tanzania hususani kusimamia kwa ukaribu ushirikiano katika maeneo ya kiuchumi.

Mhe. Rais Magufuli amewaomba Mabalozi hao kufikisha salamu zake kwa viongozi wakuu wa nchi hizo na kubainisha kuwa Tanzania ipo tayari kwa ushirikiano zaidi utakaoleta manufaa kwa wananchi wa nchi zote.

 

Wakati huo huo, Mhe. Rais Magufuli amekutana na kufanya mazungumzo na Mkurugenzi Mkuu wa Masuala ya Kimataifa wa Canada Mhe. Marc-Andre Fredette, Ikulu Jijini Dar es Salaam.

 

Baada ya mazungumzo hayo Mhe. Fredette ambaye anashughulikia Wizara 3 za Canada (Wizara ya Mambo ya Nje, Wizara ya Biashara za Kimataifa na Wizara ya Maendeleo) amepongeza maendeleo makubwa ambayo Tanzania imeyapata na amesema Tanzania na Canada zinaendelea kushirikiana katika maeneo mbalimbali yakiwemo katika sekta ya afya na elimu kwa ufanisi mkubwa.

Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Dar es Salaam
10 Desemba, 2018

UTACHEKA! JPM Alivyomkumbuka ZAKAYO wa Yesu!

Comments are closed.