Mike ampata mrithi wa Thea
Staa wa filamu za Kibongo Mike Sangu akiwa na mpenzi wake huyo mpya.
Hamida Hassan
Baada ya kimya cha muda mrefu tangu alipoachana na mkewe Salome Urassa ‘Thea’, staa wa filamu za Kibongo Mike Sangu amempata mrithi ambaye ataziba pengo.
Chanzo cha karibu na Mike kililitonya Ijumaa kuwa Mike ameamua kuingia katika uhusiano mpya na mrembo aitwaye Lizzy G wa Mwanza baada ya Thea kudai amemsahau na wala akumbuki kama aliwahi kuolewa naye.
Mike alipoulizwa kuhusu mdada huyo alikiri kamuopoa na kwamba wana mpango wa kuoana siku si nyingi.


Comments are closed.