×

Waziri Mavunde azindua tamthilia ya ‘Kelele’

2Mavunde akiongea jambo wakati wa uzinduzi huo ukumbi wa Paparazi Masaki jijini Dar es Salaam.
3Mkurugenzi Mkuu wa THT, Ruge Mtahaba, akielezea namna walivyoiandaa tamthilia hiyo.
4Baadhi ya wanamitindo wakitoa burudani kwenye uzinduzi huo.
5Msanii wa Hip Hop, Farid Kubanda ‘Fid-Q’ (katikati), akibadilishana mawazo na Mtangazaji wa Clouds FM, Adam Mchovu na Mtangazaji wa East Africa Radio, Ana Peter.
6Baadi ya waimbaji wa THT Band wakitumbuiza kwenye uzinduzi huo.

7Wasanii wanaounda kundi la Navy Kenzo, Nahreel na Aika wakifuatilia kwa makini uzinduzi huo.
8Wanamitindo wakiwa katika pozi la pamoja baada ya kumaliza kutoa burudani.
9Warembo wakiwa mbele ya kamera.
10Mwana mitindo maarufu Bongo, Ally Rehmtulah, akiwa  na mrembo.
11Mtangazaji wa Clouds TV, Shadee akiwa kwenye pozi kwenye Red Carpet.
12Mtangazaji wa Clouds FM na TV, Hamisi Dakota.
13Mtangazaji wa Clouds FM, Adam Mchovu na rafikiye.
14Vijana wanauonda kundi la Makomando wakifuatilia kwa makini uzinduzi huo.
15Baadhi ya wadau waliohudhuria uzinduzi huo wakibadilishana mawazo.1Naibu Waziri wa Kazi, Vijana na Ajira Anthony Mavunde (wa saba kutoka kushoto), akiwa kwenye pozi la pamoja na baadhi ya washiriki wa tamthilia hiyo.

NAIBU Waziri wa Kazi, Vijana na Ajira, Anthony Mavunde, usiku wa kuamkia leo amefanikisha uzinduzi wa tamthilia mpya ya Kelele, iliyoandaliwa na Taasisi ya Kuendeleza na Kukuza Vipaji (Tanzania House of Talent – THT).

Uzinduzi huo ulifanyika   ndani ya Ukumbi wa Paparazi uliopo katika Hoteli ya Slipway Masaki jijini Dar es Salaam.  Akizungumza muda mfupi kabla ya kuzindua tamthilia hiyo. Mavunde alisema kwamba, anawapongeza  THT kwa kuendelea kuisaidia serikali kwenye suala la kuwatafutia vijana ajira.

“Tunaishukuru sana THT kwa kuendelea kuiunga mkono serikali kwenye suala la kutatua na kuendelea kuongeza ajira kwa vijana wetu, tunatambua wazi kabisa kuwa serikali pekee haiwezi kumaliza tatizo hili pasipo watu binafsi kuongeza ajira kwa namna hii,” alisema Mavunde.

Kwa upande wa Mkurugenzi Mkuu wa THT, Ruge Mtahaba, alimpongeza Mavunde  kwa kuitikia wito wa kuwa mgeni rasmi wa uzinduzi wa filamu hiyo.

(NA MUSA MATEJA/GPL)

Leave a Comment