×

Nilivyoteseka Kwenye Mianzi ya Kichawi -12

Tulifanikiwa kutoka kwenye shimo la kifo salama japokuwa msichana mmoja alikuwa mgonjwa. Tulitumia siku saba kuchimba tundu la kututoa shimoni.

Niliwaacha wenzangu pale kwenye pango na kwenda kwa mkuu wa nchi ile aliyeamuru tutupwe shimoni tufe, walinzi waliponiona walinishangaa na kuingiwa na woga lakini mkuu mwenyewe pia aliponiona alipigwa na butwaa. Nilimsalimia kwa heshima zote.

“Kwani wewe ni Issa Namakoto au ni macho yangu?” aliuliza.
“Ni mimi mtukufu. Kama nilivyokueleza, mimi ni mtume wa Mungu na ndiye aliyenitoa. Kesho nitawaleta wote uliowatupa shimoni.”
Nilijifanya natoweka, nikaenda kwa wenzangu, tulilala na kesho yake tukafika kwa kiongozi yule. Tulipikiwa vyakula vya kila aina, tukala kisha wote tulirudishwa katika Bustani ya Nangose, tulikuta basi letu, tulipanda na kurudi Dar na hivyo ndivyo nilivyoteseka kwenye mianzi ya kichawi Nangose. Ilikuwa safari ya hatari!
Mwisho.

Wiki iliyopita nilipata simu na sms nyingi kutoka kwa wasomaji wangu wakihoji kwa nini hadithi ni fupi sana, niwaombe radhi kwamba tumeifupisha kutokana na sababu za kiufundi.

1 Comment

Leave a Comment