Beki wa timu yake, Hassan Kessy.
Omary Mdose na Said Ally
KIPA wa Simba, Vincent Angban, raia wa Ivory Coast, amefunguka juu ya taarifa kuwa alimpiga ngumi beki wa timu yake, Hassan Kessy mara baada ya timu hiyo kufungwa bao 1-0 na Toto Africans, Jumapili iliyopita.
Angban amesema kuwa hakufanya tukio hilo, bali walipishana kauli tu na kuwa alimkunja, tukio ambalo lilitokea kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar.
“Unajua kwenye maisha ya soka mambo kama hayo yanatokea na ni kawaida kwa wachezaji kugombana, unaweza kuona hata klabu kubwa duniani wachezaji wanagombana lengo likiwa ni moja tu, kuwekana sawa kwa ajili ya maslahi ya timu.
“Siku hiyo wakati tunaongea na Kessy baada ya kupoteza mchezo ikatokea kutoelewana na ndiyo yakatokea hayo yote, nadhani hakuna kibaya nilichokifanya, bali ilikuwa ni sehemu ya kuitetea timu,” alisema Angban.
Katika mechi hiyo, Kessy alitolewa nje kwa kadi nyekundu kwa kumfanyia faulo straika wa Toto, Edward Christopher ‘Edo’, kitendo ambacho uongozi wa klabu yake pia umekilaani na kumfungia kucheza mechi tano zinazofuata ambazo zinamaanisha hataichezea tena Simba msimu huu.
JIUNGE NA SOCIAL MEDIA ZETU:
KWA HABARI ZA KITAIFA, KIMATAIFA, MASTAA NA MIKASA YA KUSISIMUA
INSTAGRAM: @Globalpublishers
TWITTER: @GlobalHabari
FACEBOOK: @GlobalPublishers
SUBSCRIBE YOU TUBE: GlobalPublishers
GLOBAL TV ONLINE: www.globaltvtz.com
HADITHI ZA KUSISIMUA NA MBINU ZA UJASIRIAMALI, ERIC SHIGONGO FACEBOOK PAGE: @shigongotz