Mwigizaji wa Kenya, Juma Shibe ‘MJ’ (kulia), meneja wake Khalifan Ally wakiwa na mama Kanumba kwenye kaburi la mwanaye.
Stori: Mayasa Mariwata, Wikienda
DAR ES SALAAM: Tutakukumbuka daima! Mwigizaji wa Kenya, Juma Shibe ‘MJ’ akiambatana na meneja wake, Khalifan Ally, wametinga kaburini kwa aliyekuwa staa wa Bongo Muvi, Steven Kanumba kwenye Makaburi ya Kinondoni, Dar kwa lengo la kumuenzi jamaa huyo na kumfariji mama yake, Flora Mtegoa ikiwa ni miaka minne tangu kifo cha mwanaye.
Tukio hilo lililoshuhudiwa na Wikienda lilijiri mwishoni mwa wiki iliyopita ambapo jamaa hao waliambatana na mama Kanumba ambaye kama kawaida yake alikuwa akiangua kilio muda wote.
Wakiwa kaburini hapo, waliweka mashada na kumuombea marehemu ndipo mama huyo akatokwa na machozi kwa kuona vijana hao wamefunga safari kuja Bongo kwa ajili ya Kanumba.
Kwa upande wake MJ alisema: “Kanumba alikuwa mtu muhimu, alinishawishi kuingia kwenye sanaa, siku chache kabla ya kifo ilikuwa tucheze filamu ya pamoja.”
KUNUNUA NA KUSOMA MAGAZETI YA GLOBAL PUBLISHERS ONLINE, INGIA HAPA==>VODACOM M-PAPER APP
*********
JIUNGE NA SOCIAL MEDIA ZETU:
KWA HABARI ZA KITAIFA, KIMATAIFA, MASTAA NA MIKASA YA KUSISIMUA
INSTAGRAM: @Globalpublishers
TWITTER: @GlobalHabari
FACEBOOK: @GlobalPublishers
SUBSCRIBE YOU TUBE: GlobalPublishers
GLOBAL TV ONLINE: www.globaltvtz.com
HADITHI ZA KUSISIMUA NA MBINU ZA UJASIRIAMALI, ERIC SHIGONGO FACEBOOK PAGE: @shigongotz

