
Karani wa Baraza la Mawaziri, Hassan Ramadhani Shebuge (mara nyingi husimama pembeni mwa Rais wakati wa viapo), amefariki dunia.
Mwili wa Marehemu utaswaliwa leo nyumbani kwake Mbagala Majimatitu kabla ya kusafirishwa kwenda Korogwe kwa ajili mazishi yatakayofanyika hapo kesho katika kijiji cha Funta, Bumbuli mkoani Tanga.
