×

MIKANDA YA UBINGWA WA GLOBAL TV HADHARANI (Video)

Bondia wa Tanzania, Francis Miyeyusho ‘Chichi Mawe’.

KAMISHENI ya Ngumi za Kulipwa Tanza­nia (TPBO) imeiweka hadharani mikanda itakayogombaniwa katika mapambano ya Tubing wa Global TV, Afrika Mashariki na Kati yatakayofanyika Julai 22, mwaka huu kwenye Ukumbi wa Dar Live, Mbagala Zakhem, Dar.

Katika mapambano hayo ya kimataifa yat­akayorushwa mubashara na Kituo cha Global TV Online kupitia webiste yake ya www.globaltvtz. com, Bondia wa Tanzania, Francis Miyeyusho ‘Chichi Mawe’ atapambana na Is­rael Kamwamba wa Ma­lawi.

Pambano lingine litakuwa ni kati ya Idd Pi­alali dhidi ya Regin Cham­pion raia wa DR Congo, wakati Nasibu Ramadhan ‘Pacman’ atacheza na Ti­nashe Mwadziwana kuto­ka Zimbabwe. Mapamba­no hayo yote ni ya raundi kumi.

Rais wa TPBO, Yassin Abdallah ‘Ustaadh’, amei­tambulisha mikanda itakayogombaniwa katika mapambano hayo huku akithibitisha uwepo wa Balozi wa Malawi wa hapa nchini, Hawa Ndilowe kwenye pambano hilo.

“Maandalizi ya mapam­bano ya kimataifa, kati ya mabondia wa kutoka DR Congo, Malawi na Zim­babwe ambao watapi­gana na mabondia wetu hapa, yamekamilika. Kila kitu kimeshakuwa sawa na wameshapata barua maalum kutoka katika mashirikisho ya nchi zao.

“Huo ndiyo mfumo wa ngumi za kulipwa unavy­okuwa, bondia anatakiwa apate ridhaa na kibali cha kwenda kupigana nje ya nchi kutoka kwa kamish­eni, chama au shirikisho la ngumi za kulipwa ndani ya nchi yake.

Ti­nashe Mwadziwana

“Lakini jambo lingine la heshima ni kuwa nimepa­ta uthibitisho kutoka kwa ndu­gu zetu wa Malawi kuwa balo­zi wao, Hawa Ndi l owe ambaye y u p o h a p a n c h i n i atakuwe­po kush­u h u d i a n d o n g a hizo.

“ L a b d a niwaambie ma b o n d i a wa Tanza­nia ambao w a t a c h e z a katika mapam­bano hayo ya ubingwa na mabondia kuto­ka nje, najua wa­najiandaa vizuri lakini natoa onyo kwao kwamba hawa mabondia wanaokuja siyo legelege hata kidogo.

“Tumeleta mabondia wa ukweli kwa saba­bu hili pambano litaonyeshwa live kupi­tia Global TV Online maana Watanzania siku zote wanapenda vitu vizuri, vya ukweli na ha­wapendi kuona vitu feki.

“Licha ya hivyo sisi kama viongozi tupo ka­tika mipango ya kuujen­ga mchezo wa ngumi za kulipwa kwa Watanza­nia ili tujenge uaminifu zaidi kwa wadau wa mchezo huu hapa nchini, ieleweke kuwa mchezo huu ni wa pili kwa ukubwa hapa kwetu.

Mikanda Ya Ubingwa Wa Global Tv.

“Mashabiki wote ndani na nje ya nchi wajue kuwa pambano  hili halitakuwa kama ilivyo­zoeleka katika mapambano mengine.

“Kiukweli hatutahitaji watu wengi ndani ya uku­mbi kwa sababu wale am­bao watapata fursa ya kuja ndani ya ukumbi pale Dar Live watakuwa wana kadi maalum za mialiko na wen­gine ambao hawataweza kupata kadi hizo wataanga­lia kupitia Global T V On­line am­bayo itarusha mu­bashara kabisa kutokea nda­ni ya ukumbi.

“Tumeamua ku­fanya hivi ili kuwa­punguzia shida watu kutoka sehemu mbalim bali kufika ukumbini ili kuweza kuona moja kwa moja na badala yake wataweza kuangalia kila k i n achotokea ukumbini kupitia katika simu zao za mkononi.

“Sisi kama TBPO tume­omba udhamini wa Global TV na wamekubali, ni kitu cha kupongezwa, tunamshukuru sana Mku­rugenzi wa Global Publish­ers Ltd, Eric Shigongo kwa kukubali kwake pambano hili lirushwe moja kwa moja ili watu wengi waweze ku­jionea kwa urahisi kabisa maana wao ndiyo wameg­haramikia kila kitu.

“Sasa kuweza kushuhu­dia mapambano hayo ka­tika simu tena bure basi hakikisha unajiunga (sub­scribe) na YouTube Channel ya Global TV Online.

“Unachotakiwa kufanya ni kuingia YouTube, tafuta Global TV Online, kisha ub­onyeze neno SUBSCRIBE, pia ubonyeze kikengele kidogo kilichopo pembeni yake ambacho kitakukum­busha kuangalia pambano hilo mara tu litakapoanza.

“Lakini kama ume­shajiunga, basi hakiki­sha umebonyeza hicho kikengele ili usipitwe na kila kinachoendelea ndani ya Global TV. Nje ya hapo unaweza kuipata kupitia mtandao wao wa www. globaltvtz.com.

“Niwaombe mabondia wetu kuwa fursa hii ya kuweza kupata pambano hili ambalo litarushwa moja kwa moja ni kitu kikubwa sana kwao maana itasaidia kuweza kuwauza sokoni kirahisi.

“Kila mtu atakuwa ame­waona wakati wa wak­icheza bila ya kusimuliwa, nasema hivi kutokana na tayari nimeshaanza kupokea simu kutoka ka­tika baadhi ya mataifa ya Ulaya kuhusu hili pambano.

“Nataka mabondia wetu wacheze vizuri, sina wasiwasi na mabondia wanaokuja, ni wakali na wanarekodi nzuri lakini nataka mabondia wetu wacheze na wapigane kwelikweli,” anasema Us­taadh.

Katika hatua nyingine, pambano hilo, halitakuwa na kiingilio na mashabiki wataweza kulishuhudia mubashara kupitia simu zao za mkononi tu, kwani litaonyeshwa na Glo­bal TV pekee. Wadau na mashabiki watakaopata nafasi ya kuingia ukumbini wataingia kwa kadi maa­lum za mwaliko tu.

VIDEO: Mikanda Ya Ubingwa Wa Global Tv Hadharani

Leave a Comment