Mkurugenzi wa Global Publishers & General Enterprises Ltd, Eric James Shigongo (kushoto) akiongea jambo na Shaka Ssali baada ya kumaliza kufanya mahojiano na Global TV Online.Meneja Mkuu wa Global Publishers, Abdallah Mrisho (kushoto) akiwa katika picha ya pamoja na Shaka.Kutoka kushoto, Eric Shigongo, Mtangazaji wa Global TV Online, Catherine Kahabi, Shaka Ssali na Mhariri wa Ijumaa Wikienda, Sifael Paul.Wakiwa katika picha ya pamoja kabla ya kuondoka ofisi za Global Publishers, Bamaga Mwenge jijini Dar.
MTANGAZAJI wa kimataifa kutoka Idhaa ya Kiswahili ya Sauti ya Amerika (VoA) ambaye ni mhariri na mtangazaji wa Kipindi cha Straight Africa Talk, Shaka Ssali mapema leo ametembelea Ofisi za Global Publishers na kufanya mahojiano maalum.
Mbali na mambo mengine, Shaka amewahimiza wafanyakazi wa Kampuni ya Global Publishers, kutanguliza uzalendo katika kazi zao na kujifunza mambo mapya kila kukicha.