×

NBC Yatoa Mafunzo Kwa Wafanyabiashara Dar

Mkuu wa Kitengo cha Wafanyabiashara wa Kati na Wadogo wa Benki ya NBC, Evance Luhimbo akizungumza na wafanyabiashara  wadogo na wa kati wa maeneo ya Kariakoo, katika semina ya siku moja iliyoandaliwa na benki hiyo kwa lengo la kuwawezesha kimafunzo yatakayosaidia katika ukuaji wa biashara zao jijini Dar es Salaam jana.
Meneja Maendeleo ya Viwanda wa Chama cha Wafanyabiashara, Viwanda na Kilimo Tanzania (TCCIA), Patrick Magai akitoa elimu kuhusu fursa za viwanda katika semina ya siku moja iliyoandaliwa na benki ya NBC kwa wateja wake wafanyabiashara wadogo na wa kati wa maeneo ya Kariakoo jana.
Msaidizi wa Msajili Mkuu wa Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA), George Chuwa akizungumza katika semina ya siku moja iliyoandaliwa na benki ya NBC kwa wateja wake wafanyabiashara wadogo na wa kati wa maeneo ya Kariakoo jiijini Dar es Salaam jana.
Ofisa Msimamizi wa Walipa Kodi wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Joyce Ng`oja akitoa elimu kuhusu kodi katika semina ya siku moja iliyoandaliwa na benki ya NBC kwa wateja wake wafanyabiashara wadogo na wa kati wa maeneo ya Kariakoo jijini Dar es Salaam jana.
Mkurugenzi wa Biashara wa NBC, Elvis Ndunguru (wa pili kushoto) akizungumza jambo na wafanyabiashara wadogo na wa kati wa maeneo ya Kariakoo jijini Dar es Salaam wakati wa semina iliyoandaliwa na benki hiyo yenye lengo la kuwawezesha kimafunzo kuhusu ukuaji wa biashara zao jijini humo jana.

Leave a Comment