×

Makonda Aanika Akavyoishi Mtaani Baada ya Kuwa RC – Video

ALIYEKUWA Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda amekabidhi rasmi ofisi hiyo kwa Mkuu wa Mkoa Mpya wa Dar, Aboubakar Kunenge, leo Jumatatu, Agosti 3, 2020 katika ofisi hizo zilizopo Ilala, jijini Dar es Salaam.

 

Akizunumza wakati wa kukabidhi ofisi hiyo, Makonda amesema:

 

“Kazi ya uteuzi siyo rahisi ina taarifa na maelezo mengi, lakini Rais Magufuli aliamini katika vijana, nikiwa kijana wa kwanza kupewa majukumu katika mkoa mkubwa na kuacha alama itakayodumu milele yote. Ningekuwa ni jeshini ninazo medali za kivita ni askari mmoja aliyepo back bencher mwenye uwezo mkubwa wa kupigana vita yoyote.

 

“Kwa hiyo Mheshimiwa  RC, Mambosasa na timu yenu mkihitaji uzoefu wangu katika mapambano ya kumlinda Dkt John Pombe Magufuli, hata kama ni saa tisa usiku nitaamka. Kwangu yeye ni zaidi ya cheo, ni baba.

“Nina kila sababu ya kumshukuru mke wangu, kipenzi changu Maria, amenivumilia sana, lakini pia ameniombea, ‘mme wangu nilidhani maneno yameisha baada ya kuacha ofisi, mbona bado yapo mengi tu?’ Mimi nikamwambia, maneno ndiyo mtaji wangu, kusemwa ndiyo furaha yangu, nisiposemwa mpaka najiuliza leo kuna nini mitandao imekaa kimya, hawawezi kukusema kama hauna jambo la maana na kazi yako kubwa ni kumtanguliza Mungu

 

“Nimshukuru sana mke wangu Maria na mwanangu kipenzi Keagan kwa kuendelea kuwa wavumilivu na kuvumilia masimango na maneno ya hovyo na machafu yaliyotamkwa juu yao na familia yangu katika kipindi chote cha utumishi wangu na yatakayoendelea.

 

“Nasema haya kwa sababu naaga, sitegemei tena kurudi katika nafasi hii kwenye ofisi hii, nikija hapa basi nitakuja kama mwananchi wa kawaida na nitapanga foleni pale. Na wala msisite na maneno ya watu ya kwamba ataishije, ataenda wapi, mngeumia zaidi siku mkisikia Makonda amemuacha Yesu, Lakini maadamu Yesu ninaye, msiwe na shaka na mimi maisha yangu yapo salama.

 

“Tulipanga Mzee Pengo tumpe barabara na tangu mwaka jana tulikuwa tumkabidhi barabara na jana nilipita kuiangalia nikakuta kuna kibao kimewekwa, ningefurahi kwa heshima yake tumkabidhi ile barabara na ijulikane kama Kardinali Pengo Road.
“RC endelea na huduma za afya kila mwaka, kwa ajili ya wajane, maskini, walemavu, lakini kuliko yote lile la watoto wanaotelekezwa na tulipeleka mapendekezo kwa Waziri wa Katiba na Sheria pamoja na mapendekezo ambayo yapo tayari.
“Mwendo nimeumaliza, imani na kiapo changu cha utumishi nimekikamilisha kikamilifu, sasa wana Dar es Salaam mniruhusu nikapumzike kwa amani katika utumishi wangu kwa kumlea mke wangu kipenzi Maria na mtoto wangu Keagan.”

Leave a Comment