BWENI la Shule ya Sekondari ya African Muslim iliyopo maeneo ya Kaloleni mkoani Kilimanjaro limeungua moto huku chanzo cha moto huo kikiwa hakijafahamika.
Kwa mujibu wa mkaguzi wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji mkoani Kilimanjaro, Jeremiah Mkomangi, hakuna majeruhi wala kifo, ila vitu mbalimbali, vikiwemo vitanda vimeteketea.
Amesema moto huo ulianzia kwenye chumba ambacho kinatumika kama stoo.
