
MHASHAMU Askofu Mkuu wa Kanisa Katoliki Jimbo Kuu Dar es Salaam, Jude Thadeus Ruwa’ichi ameipongeza Benki ya ACB na wadau wengine kwa kuiwezesha Shule ya Mary Mother of Mercy kwa kuwahifadhia fedha na kuikopesha hali iliyopelekea mafanikio makubwa iliyo nayo sasa.

Ruwachi alisema hayo kwenye uzinduzi wa shule hiyo iliyopo shule hiyo ya mtaala wa kiingereza iliyopo Gongo la Mboto, Mji Mpya, Jijini Dar ambapo alikuwa akiwasifu watu na taasisi mbalimbali zilizofanikisha maendeleo ya shule.

Sambamba na uzinduzi rasmi wa shule hiyo kulikuwa na mahafali ya kwanza ya darasa la saba na darasa la awali.
Benki ya ACB kama wadau wa shule hiyo wamekuwa wakihifadhi pesa za shule hiyo pamoja na kuikopesa pesa kwa ajili ya maendeleo yake.

Katika mahafali hayo benki hiyo ilimzawadia kiasi fulani cha pesa pamoja na kumfungulia akaunti mwanafunzi Gerald Kyaruzi ambaye aliwaongoza wenzake kwenye mitihani ya mwisho kuelekea mtihani wa taifa iliyofanywa shuleni hapo.

Meneja wa ACB Tawi la Banana Ukonga, Agnes Nyakali ndiye aliyemkabidhi kitita mhitimu huyo kitita hicho na kisha kumfungulia akaunti kwenye benki hiyo akishuhudiwa na Mkuu wa Kitengo cha Masoko katika benki hiyo, Innocent Ishengoma pamoja na wageni waalikwa wengine. HABARI/PICHA NA RICHARD BUKOS /GPL