
PEP Guardiola anaamini kuwa kocha wa Arsenal, Mikel Arteta ataimarika na kuwa bora na kikosi chake msimu ujao. Arteta kabla ya kutua Arsenal alikuwa msaidizi wa Guardiola katika kikosi cha Manchester City ambacho msimu huu kimeibuka kuwa mabingwa wa Premier.
Arsenal kwa sasa ipo nafasi ya tisa kwenye msimamo wa Premier, baada ya mechi 36 ikiwa imekusanya pointi 55. Msimu huu, Arteta imeshindwa kutamba kwani iliondolewa kwenye FA na ikishia hataua ya Nusu Fainali ya Europa League dhidi ya Villarreal.
Guardiola alisema anaamini kuwa Arteta atafanya vizuri kwani ni kocha bora na anahitaji muda tu. “Arsenal inatakiwa kumuamini Mikel hasa kuelekea msimu ujao mimi ninamfahamu vizuri naamini atakuwa bora zaidi msimu ujao.
“Ukiangalia klabu nyingi kwa msimu huu zilipambana kucheza vizuri na ushindani kuwa mgumu na kupitia kipindi kigumu kwa hii misimu miwili mfululizo.”
Arteta ameiongoza Arsenal katika mechi 84 tangu alipopewa kazi ndani ya klabu hiyo akipokea kutoka kwa Unai Emery na amefa-nikiwa kutwaa taji la Kombe la FA msimu uliopita pamoja na Ngao ya Jamii.
MANCHESTER, England