×

‘Bwam’dogo’ wa Uwoya Dubai Gumzo

BATA analokula msanii Irene Uwoya, Dubai, Falme za Kiarabu, tangu Juni 22, mwaka huu alipotinga huko, linaendelea kuwaunguza wenye roho za korosho.

 

Habari iliyoibuliwa hivi sasa inamhusu mwanaume mmoja anayeonekana kuwa Bwam’dogo fulani kuwa ndiye anayedhamini ‘fujo’ za Uwoya huko kwenye mji wenye starehe za kila aina.

Wachunguzi wa ndani wa jungu la udaku wanasema, wamefuatilia nyendo za Uwoya na mwanaume huyo kwa muda mrefu na kugundua kuwa; mara kadhaa Uwoya na mwanaume huyo wamekuwa wakionekana pamoja au kupiga picha katika mazingira yanayofanana kwa kila kitu.

Vipi jamaa ndiyo mmiliki? Hilo limekuwa swali la wengi ambapo wengine wanasema “ndiyo” na baadhi wanasema “hapana” huku kiambatanisho cha maneno ya kitoto kwamba huyo ni “kondakta” tu; kikiwekwa na kwamba mwenye gari yuko sehemu katulia.

 

Uwoya we bwana endelea kujilia vyako hayo maneno kwamba uko huko kwa ufadhili wa wahisani wenye hisani kubwa achana nayo, tehe, tehee, teheeee!

CC: @manyota_rich

Leave a Comment