
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa ameridhishwa na ujenzi wa daraja la JPM linalounganisha Wilaya ya Sengerema na Misungwi mkoani Mwanza ambapo amemuagiza Naibu Waziri wa Ujenzi kufanya kikao na wafanyakazi wa ujenzi wa daraja hilo kutokana na baadhi ya wafanyakazi kuacha kazi na kwenda katika ujenzi wa SGR

Akiwa Sengerema, Waziri Mkuu amezungumza na Mbunge wa Jimbo la Buchosa, Eric Shigongo kuhusu masuala mbalimbali zikiwemo kero za wananchi wa wilaya hiyo na Jimbo la Buchosa.