×

Waziri wa Ardhi afunga Masijala ya Ardhi ya Jiji la Dodoma kuondoa changamoto

Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Jerry Silaa (Kulia) akifunga kufuli kwenye ofisi ya Masijala ya Ardhi ya jiji la Dodoma alipokwenda kuzifunga rasmi ofisi hizo tarehe 28 Mei 2024.

Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Jerry Silaa amefunga Masijala ya Ardhi ya Jiji la Dodoma ikiwa ni hatua ya wizara yake kuondoa changamoto za sekta ya ardhi katika jiji la Dodoma.

Akizungumza na wananchi baada ya kufunga makufuli kwenye masijala ya ofisi ya ardhi jiji la Dodoma Mei 28, 2024, Silaa amemuelekeza katibu mkuu wa wizara hiyo kusimamia shughuli hiyo ili kuhakikisha watu wanapata haki zao.

 Jerry Silaa (Kulia) akimkabidhi fungua Katibu Mkuu Mhandisi Anthony Sanga mara baada ya kuzifunga ofisi.
Jerry Silaa (Katikati) akizungumza na wananchi mara baada kufunga ofisi ya Masijala ya Ardhi ya jiji la Dodoma.
…Jerry Silaa AKIENDELEA kuzungumza na wananchi.

 

View this post on Instagram

 

A post shared by globalpublishers (@globaltvonline)

Leave a Comment