
Rais Samia Suluhu Hassan amewatakia heri Watanzania wote katika kuadhimisha Miaka 62 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar, leo Januari 12, 2026.
Rais Samia ametuma salamu hizo kupitia mtandao wake wa Instagram akiandika; “Kwa miaka 62 tumeendeleza dhamira ya msingi ya Mapinduzi ya kujenga jamii ya watu huru, yenye utu, yenye maendeleo, umoja, haki, amani na mshikamano.”
Aidha, Rais Samia amewataka Watanzania kuendelea kuzilinda tunu za Mapinduzi na kuzirithisha kwa vizazi vijavyo.
