Vodacom Tanzania Yazindua Duka Jipya Dodoma
Afisa Mtendaji Mkuu wa Vodacom Tanzania PLC Philip Besiimire ( wa pili kushoto) akikata utepe kuashiria ufunguzi wa duka jipya la Vodacom jijini Dodoma, ikiwa na lengo la kusogeza huduma za kampuni hiyo karibu na wateja wa jiji hilo. Tukio hilo lilishuhudiwa na Mkuu wa kanda ya kati, Chiha Nchimbi (wa pili kulia) pamoja na Mdau wa Vodacom Emmanuel Makaki ( Kushoto) jana jijini Dodoma.
Mkurugenzi Mtendaji wa Vodacom Tanzania, Philip Besiimire (wa pili kulia) akisikiliza maelezo kutoka kwa mmoja wa watoa huduma wa duka jipya kubwa la Vodacom mkoani Dodoma baada ya kulizindua jana. Kulia ni Mdau wa Vodacom, Emmanuel Makaki, Mkuu wa Vodacom Kanda ya Kati, Chia Nchimbi (kulia kwake) na wafanyakazi wa kampuni hiyo.



