×

Rubani Atuhumiwa Kurusha Ndege Miaka 17 Bila Kuwa na Leseni Halali

Mamlaka za Canada zimesema rubani wa zamani wa shirika la ndege la Air Canada anatuhumiwa kusafirisha maelfu ya abiria kwa miaka 17 bila leseni halali ya urubani.

Polisi walisema ilibainika kuwa Jeffrey Wall, mwenye umri wa miaka 59 kutoka Ontario, alikuwa akirusha ndege kwa kutumia vyeti bandia tangu alipopandishwa cheo kuwa rubani mwaka 2009, na sasa anakabiliwa na mashtaka kadhaa ya ulaghai.

Air Canada ilisema rubani huyo alifukuzwa kazi mara moja baada ya kugundulika kwa udanganyifu huo mwaka jana, na ikaongeza kuwa iliripoti tukio hilo kwa hiari kwa mamlaka ya usafiri wa Canada.

Shirika hilo la ndege lilisisitiza kuwa usalama wa abiria haukuwahi kuathiriwa na kwamba marubani wote hupitia mafunzo na mazoezi ya mara kwa mara kila baada ya miezi sita.

Naibu mkuu wa polisi wa eneo la Peel kusini mwa Ontario, Nick Milinovich, alisema Bw. Wall alikuwa akifanya kazi na Air Canada kwa miaka 27, kuanzia mwaka 1998.

Leave a Comment