×

Rais Samia Ahutubia Mkutano wa AU Kuhusu Afya Ghana – Picha

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan akizungumza katika Mkutano Maalum wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Umoja wa Afrika (AU) kuhusu Afya, katika hoteli ya Elisa, jijini Accra, Ghana, tarehe 22 Julai, 2026.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amehutubia Mkutano Maalum wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Umoja wa Afrika (AU) kuhusu afya uliofanyika katika Hoteli ya Elisa, jijini Accra nchini Ghana, Julai 22, 2026.

Mkutano huo umewakutanisha viongozi wa nchi mbalimbali za Afrika kujadili namna ya kuimarisha mifumo ya afya barani, kuongeza uwezo wa kukabiliana na milipuko ya magonjwa, pamoja na kuimarisha ushirikiano katika utoaji wa huduma bora za afya.

Ushiriki wa Rais Samia unaonesha dhamira ya Tanzania ya kuendelea kushirikiana na mataifa mengine ya Afrika katika kutafuta suluhisho endelevu kwa changamoto za sekta ya afya na kuendeleza ajenda ya afya kwa maendeleo ya bara la Afrika.

Rais Dkt. Samia akiwa na Rais wa Jamhuri ya Ghana,  John Dramani Mahama, Mwenyekiti wa Umoja wa Afrika (AU) na Rais wa Jamhuri ya Burundi, Evariste Ndayishimiye, kwenye picha na viongozi mbalimbali waliohudhuria hafla ya ufunguzi wa Mkutano Maalum wa Umoja wa Afrika kuhusu Afya, jijini Accra, Ghana, tarehe 22 Julai, 2026.

Leave a Comment