Shughuli ya mtoto wa Diamond Platnumz na Zuchu imefanyika usiku wa kuamkia leo Jumapili Septemba 13, 2026 katika Ukumbi wa St. Laurent, Kawe jijini Dar es Salaam, huku hali ya furaha na shamrashamra ikitawala katika tukio hilo.
Tukio hilo limewakutanisha watu mbalimbali, wakiwemo wasanii, ndugu, marafiki na wageni waalikwa, ambao wamejitokeza kushiriki katika siku hiyo maalum.
Ukumbi wa St. Laurent umeonekana kupambwa kwa ajili ya shughuli hiyo, huku wageni wakifurahia pamoja na familia katika mazingira yaliyojaa furaha na bashasha.
Diamond na Zuchu, ambao ni miongoni mwa majina makubwa katika muziki wa Tanzania, wameendelea kuvuta hisia za mashabiki kila wanapoonekana pamoja katika matukio mbalimbali.
Kwa upande wa mashabiki, tukio hilo limekuwa gumzo mitandaoni, huku picha na video mbalimbali zisambaa kwenye mitandao zikionyesha namna shughuli hiyo inavyokwenda.