×

Singida Black Stars Yathibitisha Mabadiliko ya Uongozi wa Klabu

Uongozi wa Klabu ya Singida Black Stars umetangaza mabadiliko ya uongozi baada ya Mtendaji Mkuu wa Klabu hiyo, Ndg. Kassano Jonathan, kuomba kujiuzulu nafasi yake.

Kupitia taarifa iliyotolewa leo Septemba 13, 2026, uongozi wa klabu umesema umekubali ombi hilo na kumteua Ndg. Tabitha Kidawawa kuwa Mtendaji Mkuu mpya wa Singida Black Stars, akisaidiwa na Naibu wake, Muhibu Kanu.

Aidha, uongozi wa klabu umemshukuru Kassano Jonathan kwa mchango wake mkubwa katika kipindi chote alichohudumu, huku ukimtakia kila la heri katika hatua zake zijazo.

Uongozi umeeleza kuwa unaamini mabadiliko hayo yataisaidia Singida Black Stars kuendelea kuwa nyumbani kwa wanyumbani wake na kufikia malengo yake.

Leave a Comment