×

Tulia Ackson Amfariji Rais Samia Baada ya Msiba wa Mumewe – Picha

Aliyekuwa Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mbunge wa Jimbo la Uyole, Tulia Ackson, amemfariji Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, baada ya kuwasili nyumbani kwake Kizimkazi, Mkoa wa Kusini Unguja, Zanzibar.

Tulia amefika Kizimkazi kufuatia msiba wa mume wa Rais Samia, Marehemu Maalim Hafidh Ameir Hassan, aliyefariki dunia katika Hospitali ya Kumbukumbu ya Emilio Mzena Zanzibar, Septemba 7, 2026.

Katika kipindi hiki cha majonzi, viongozi, ndugu, jamaa na Watanzania mbalimbali wameendelea kutoa pole na kushirikiana na Rais Samia pamoja na familia yake katika kuomboleza msiba huo.

Marehemu Maalim Hafidh Ameir Hassan ameacha pengo kubwa kwa familia na watu waliokuwa karibu naye.

 

Leave a Comment