×

Zanzibar: Wajumbe wa Kamati ya Pamoja CCM na ACT Wazalendo Watangazwa

Serikali ya Mapinduzi Zanzibar kupitia Ofisi ya Baraza la Mapinduzi imetangaza majina ya Wajumbe wa Kamati ya Pamoja ya Majadiliano kati ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) na Chama cha ACT Wazalendo.

Hatua hiyo inafuatia makubaliano yaliyofikiwa na vyama hivyo viwili tarehe 9 Julai 2026, ambapo vilitia saini Tamko la Pamoja la Makubaliano kuhusu Ajenda za Kufanyiwa Kazi katika hafla iliyofanyika Ikulu, Zanzibar.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa Septemba 13, 2026, Kamati hiyo imeundwa na wajumbe 10, ambao ni:

  1. Ndg. Abdi Mahmoud Abdi – Mjumbe na Mwenyekiti Mwenza wa Kamati
  2. Ndg. Omar Ali Shehe – Mjumbe na Mwenyekiti Mwenza wa Kamati
  3. Mhe. Dkt. Khalid Salum Mohamed – Mjumbe
  4. Mhe. Najma Murtaza Giga – Mjumbe
  5. Mhe. Masoud Ali Mohamed – Mjumbe
  6. Mhe. Mgeni Hassan Juma – Mjumbe
  7. Ndg. Omar Said Shaaban – Mjumbe
  8. Ndg. Fatma Abdulhabib Fereji – Mjumbe
  9. Mhe. Said Ali Mbarouk – Mjumbe
  10. Ndg. Mohamed Nur Mohamed – Mjumbe

Aidha, Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi amewateua Makatibu na Sekretarieti ya Kamati hiyo kama ifuatavyo:

Makatibu wa Kamati

  1. Ndg. Mwalim Ali Mwalim
  2. Ndg. Seif Khamis Mohamed

Sekretarieti ya Kamati

  1. Ndg. Hamid Saleh Mhina
  2. Ndg. Mohamed Yusuf Nuh
  3. Ndg. Ali Salim Khamis
  4. Ndg. Abdalla Mussa Hijja

Kamati hiyo inatarajiwa kuanza rasmi majukumu yake siku ya Jumatatu, tarehe 14 Septemba 2026, saa 5:00 asubuhi, Ikulu Zanzibar.

Leave a Comment