
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan, amepiga simu live katika Kongamano la Mafunzo ya Uongozi na Fursa za Kiuchumi kwa Viongozi wa Shirikisho la Umoja wa Machinga.

Rais Samia amesema katika Bajeti ya mwaka wa fedha 2022/2023 utakaoanza Julai mwaka huu, Serikali itatoa Shilingi milioni 10 kila Mkoa kwa ajili ya uendeshaji wa Ofisi za Machinga.