The House of Favourite Newspapers

BEYONCE, KIM KARDASHIAN KUNA NINI TENA???

0

MSANII kutoka Marekani ambaye pia ni mke wa Rapa Jay Z, Beyonce Knowles ameibuka gumzo mitandaoni baada ya kukataa zawadi alizoletewa na Mwanamitindo maarufu nchini humo Kim Kardashian, kwa ajili ya watoto wake mapacha aliojifungua mwezi uliopita.

Kim Kardashian ambaye ni mke wa Rapa Kanye West, aliandaa zawadi zenye thamani ya dola 150,000 na kuziwasilisha hospitalini alipokuwa amelazwa Beyonce kwa ajili ya matibabu ya watoto hao waliokuwa wanasumbuliwa na maradhi madogo madogo baada ya kuzaliwa, lakini baada ya kupokea zawadi hizo, alizigawa zote kwa wafanyakazi wa hospitali hiyo.

Baada ya tukio hilo, Kim alimkabidhi tena msanii huyo zawadi ya nguo alizozitoa kwenye kampuni yake ya nguo kwa ajili ya mtoto wake wa kwanza anayeitwa Blue Ivy, Lakini Beyonce alipokea zawadi hizo na kuzigawa tena kwa manesi wa hospitali hiyo wawapelekee watoto wao wakavae.

Matukio hayo mawili yamezua sintofahamu kwa mashabiki wao na watu wa karibu wa familia hizo, kuwa labda kuna ugomvi unaoendelea kati yao ,na walipotafutwa kila mmoja kwa wakati wake ili waweke mambo hadharani juu ya kinachoendelea kati yao , wote wamekataa kuzungumzia.

Leave A Reply