Mkuu wa Jeshi la Libya afariki katika ajali ya ndege nchini Uturuki

Waziri Mkuu wa Libya ametangaza kwamba Mkuu wa Jeshi la nchi hiyo, Jenerali Mohammed Ali Ahmed al-Haddad, amefariki katika ajali ya ndege iliyotokea nchini Uturuki.
Taarifa zinaeleza kuwa Jenerali al-Haddad alikuwa ndani ya ndege ya biashara aina ya Falcon 50 pamoja na watu wengine wanne, wakitokea Ankara, Jumanne jioni.

Kupitia chapisho kwenye mtandao wa X, Waziri wa Mambo ya Ndani wa Uturuki, Ali Yerlikaya, alisema mawasiliano na ndege hiyo yalipotea saa 20:52 kwa saa za eneo — takribani dakika 42 baada ya kupaa kutoka Uwanja wa Ndege wa Ankara. Kabla ya tukio hilo, rubani aliripotiwa kuomba ruhusa ya kutua kwa dharura.
Mabaki ya ndege yalipatikana eneo la kusini-magharibi mwa Ankara, na mamlaka za Uturuki zimethibitisha kuwa uchunguzi rasmi umeanza ili kubaini chanzo cha ajali.

