×

RC Makalla Awaapisha Fatma Nyangasa na Kheri James-Picha

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Amos Makalla akimwapisha Mkuu wa Wilaya ya Ubungo, Kheri James.
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Amos Makalla akimwapisha, Fatma Almass Nyangasa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Kigamboni.
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Amos Makalla akizungumza jambo.

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam  Amos Makallaleo June 21 amewaapisha Wakuu wapya wa Wilaya za Kigamboni na Ubungo walioteuliwa na Rais wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan  mwishoni mwa Wiki.

Wakuu wa Wilaya walioapishwa na RC Makalla ni pamoja na  Kheri James alieyapishwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Ubungo pamoja na Mhe.Fatma Almass Nyangasa aliyeapishwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Kigamboni.

Akizungumza wakati wa kuwaapisha Viongozi hao RC Makalla amewataka Viongozi hao kuhakikisha wanatekeleza majukumu yao ipasavyo ikiwa ni pamoja na kusimamia ukusanyaji wa Mapato, kushughulikia kero za Wananchi, ulinzi na usalama, Usafi na usimamizi wa miradi ya maendeleo.

Leave a Comment