Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dk Emmanuel John Nchimbi amesema kuwa kupitia juhudi za Mhe. Dkt. Samia Suluhu za kuendelea kuleta maendeleo kwa wananchi hazitawafanya wananchi kubezi juhudi hizo na hivyo wataendelea kutangaza mema yanayoonekana.
Wanachama, Viongozi wa CCM wa ngazi mbalimbali na wawakilishi wa makundi mengine, wamejitokeza kwa wingi kufuatilia kwa makini hotuba ya Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dk Emmanuel John Nchimbi alipokutana na kuzungumza nao kwenye mkutano wa ndani uliofanyika mjini Singida, Mei 30, 2024, ikiwa ni mwendelezo wa vikao na mikutano ya ndani na hadhara anayofanya kwenye ziara yake mkoani humo, aliyoanza Mei 29, 2024.




