×

Video: Trump Aipa Iran Onyo Baada ya Mashambulizi ya Wahouthi Yemen

Rais wa Marekani, Donald Trump

Rais wa Marekani, Donald Trump, leo Julai 23, 2026 ameonya kuwa iwapo waasi wa Houthi nchini Yemen wataendelea kufanya mashambulizi dhidi ya meli au malengo mengine, Marekani itaishikilia Iran kuwajibika na huenda ikachukua hatua kali za kijeshi dhidi ya Tehran.

Katika ujumbe aliouchapisha kwenye mtandao wake wa Truth Social, Trump amesema kuwa mwaka mmoja uliopita Marekani ilichukua hatua za kijeshi dhidi ya Wahouthi baada ya kundi hilo kushambulia meli za kibiashara na kusababisha usumbufu katika biashara ya kimataifa.

Trump amesema Wahouthi wameanza tena mashambulizi, akidai kuwa usiku uliopita kundi hilo lilifyatua risasi dhidi ya ndege mbili za Saudi Arabia.

Rais huyo wa Marekani ameonya kuwa endapo mashambulizi kama hayo yataendelea, Iran itawajibishwa kwa kile anachodai kuwa ina uhusiano wa moja kwa moja na Wahouthi.

“Wahouthi ni vibaraka na washirika wa Iran,” Trump amesema, akiongeza kuwa iwapo hali itaendelea kama ilivyo sasa, Marekani inaweza kuchukua hatua kali dhidi ya kundi hilo pamoja na Iran.

Hata hivyo, Wahouthi wamekuwa wakikanusha madai kwamba wao ni vibaraka wa Iran, wakisisitiza kuwa wanafanya maamuzi yao wenyewe.

Leave a Comment