Ruge Afunguka Jinsi RC Makonda Alivyovamia Clouds TV Usiku na Bunduki
Vilevile Ruge ameeleza kuwa amesikitishwa sana na kitendo alichokifanya rafiki yake Paul Makonda kwani kilikuwa ni kitendo cha kuivunjia heshima Clouds Media Group pamoja na wadau wengine.
“Makonda tumesaidiana sana tangu akiwa mkuu wa Wilaya. Kwa nini leo anafika kuja ofisini kwangu na bunduki?” alisema.
Pamoja na hayo aliongeza kuwa, wao kama Clouds Media Group hawana ugomvi na serikali na ameahidi kutoa nafasi kwa kiongozi yeyote mwenye ajenda ya maendeleo kuja Clouds na atapewa muda wa kuzungumza.
“Sisi tunatafuta viongozi wabunifu. Viongozi wanaokuja na mipango inayoweza kumwezesha mnyonge kuuona mwanga. Viongozi wanapaswa kufanya mijadala ya namna ya kuongeza maendeleo. Inapaswa tushirikiane kutengeneza timu moja na kushirikiana.”
Mkurugenzi Ruge Mutahaba, alimaliza kwa kusema kuwa amelizungumzia jambo hilo leo ili limalizike na watu waendelee kufanya mambo mengine ya kuisaidia nchi kimaendeleo.
Vilevile amewataka viongozi na wanasiasa kutokushindana kupata ‘kiki’ kupitia vyombo vya habari na mitandao ya kijamii.
Comments are closed.