Katika barua iliyotolewa na Mkuu wa Kitengo cha Huduma kwa Umma, kwenda kwa Wanachama wa MAT (Multi Agency Team) imesema Serikali hiyo inatani kutengeneza sanitizer zitakazoweza kununuliwa na Watu wote.
Kitengo hicho kimesema Kampuni katika sekta ya Mafuta yamejitolea kutengeneza sanitizer zenye kiwango cha kilevi kinachotakiwa na kuzisambaza bure kwa Umma.
Katika barua hiyo MAT wametakiwa kutafuta vilevi vyote aina ya ethanol vinazoshikiliwa katika bandari mbalimbali na katika maeneo mbalimbali katika Jamhuri ya Kenya.
Pia, wametakiwa kupeleka vilevi hivyo katika Kampuni ya Kenya Pipeline (KPC) kwa kuzingatia Kanuni za Utendaji kazi wa MAT.
KPC watashirikiana na Kampuni za mafuta zilizoonesha nia ya kutengeneza Sanitizers hizo katika hali ya faida kwa wote na watatengeza mpango kazi kuhakikisha ethanol inatumika vema na Sanitizer zinagaiwa baada ya kutengenezwa.


