Mrembo kunako Bongo Muvi ambaye pia ni mzazi mwenzie na Mbunge wa Mbeya Mjini Joseph Mbilinyi ‘Sugu’, Faiza Ally amefunguka kuwa kati ya vitu ambavyo havipendi katika ujauzito wake huu ni kumuanika baba kijacho wake.
Akipiga stori na Star Mix, Faiza alisema kuwa, anafurahi kuwa mama mtarajiwa wa mtoto wake pili lakini linapokuja suala la kupiga naye picha ama kumuanika baba kijacho wake mitandaoni kama wafanyavyo wasanii wengine kwake halina nafasi.
“Kwanza nalipenda tumbo langu likiwa imejaa (ujauzito) lakini pia hakuna kitu ninachokiogopa kwa sasa kama kumuanika baba kijacho wangu ambaye yupo nje ya nchi kwa sasa naogopa wasije mkwapua bure, hayo mambo sijui ya kuuza sura naawaachia hao wasanii wengine,” alisema Faiza ambaye mtoto wake wa kwanza amezaa na Sugu.
Na Imelda Mtema |GAZETI LA IJUMAA
[…] Esha amejifungua mtoto wa kike leo, katika hospitali ya Sali International iliyopo ushuani Masaki. Na kupitia ukurasa wake wa Instagram amethibitisha taarifa hizo kwa kupost picha ya kichanga chake na kuandika maneno yafuatayo. […]