
Zlatan Ibrahimovic akishangilia bao lake la 9 kwenye EPL Msimu huu.

Kocha wa Sunderland, David Moyes (kulia) akisalimiana na Kocha wa Man U, Jose Mourinho baada ya mechi kuisha.

Goli la Mkhitaryan linafananishwa na mkwaju aliouokoa Rene Higuita kutoka kwa Jamie Redknapp kwenye Uwanja wa Wembley mwaka 1995

MANCHESTER; KLABU ya Manchester United jana Desemba 26, 2016 ilikuwa nyumbani, Old Trafford kuikaribisha Sunderland inayonolewa na aliyekuwa kocha wa Man U kabla ya kutimuliwa, David Moyes ambapo Man U walifanikiwa kuibuka na ushindi wa bao 3-1 huku Zlatan Ibrahimovic akitoa assists mbili na kutupia kambani moja.
Goli la 3 na la kipekee kwa staili ya ufungujai aliyotumia Mkhitaryan, limekuwa gumzo mitandaoni wakati mwenyewe akilipa jina kuwa ‘Scorpion’ (Nge) huku likifanananishwa kabisa na mkwaju aliouokoa Rene Higuita kutoka kwa Jamie Redknapp kwenye Uwanja wa Wembley mwaka 1995.
Mkhitaryan amesema kuwa bao hilo ni miujiza ya Krismasi kwake ambapo alifunga kwa kupiga kutumia unyayo wake wakati ikionekana kama mpira umempita.
Wanaojadili wamekuwa wakijadili mambo mawili. Wako wanaosema ni offside na wengine wamekuwa wakizungumzia ubora wake na kumpongeza Mkhitaryan ambaye asili yake ni Armenia.
Licha ya hivyo, Kocha David Moyes wa Sunderland amelalamikia bao hilo akisema kuwa, Mkhitaryan alikuwa offside wakati akifunga bao hilo.
Ushindi wao wa 3-0 dhidi ya Bournemouth uliwafanya kuweka rekodi ya klabu hiyo kushinda michezo 12 mfurulizo ya Premier League huku wakizidi kujikita kileleni mwa ligi hiyo.
Manchester City walijivuta nafasi ya pili baada ya kushinda 3-0 dhidi ya Hull City, huku Arsenal ikipata ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Wesst Brom 1-0, bao lililofungwa na Olivier Giroud.
Msimamo wa EPL
Manchester United (4-2-3-1): De Gea 6; Valencia 6.5, Jones 6.5, Rojo 6, Blind 7; Herrera 7 (Fellaini 84), Carrick 6.5; Mata 6.5 (Martial 74), Pogba 8, Lingard 6 (Mkhitaryan 62, 7.5); Ibrahimovic 7.
Subs not used: Smalling, Rashford, Romero, Darmian.
Goals: Blind 39, Ibrahimovic 82, Mkhitaryan 86
Booked: Blind
Sunderland (4-2-4-2): Pickford 6.5; Jones 6, Kone 5.5, Djilobodji 5.5, Van Aanholt 6.5; N’Dong 6 (Love 86), Denayer 6.5, Larsson 6 (Kharzi 82), Borini 7; Anichebe 7, Defoe 6.5.
Subs not used: Mannone, O’Shea, Asoro, Honeyman, Embleton.
Goal: Borini 90+1
Referee: Martin Atkinson 5.5 (W Yorkshire)
Star man: Paul Pogba.