
DAR ES SALAAm: DROO ya kwanza ya bahati nasibu ya Shinda Nyumba awamu ya pili itachezwa leo katika Viwanja vya Mbagala Zakhem, jijini Dar ambapo washindi watajipatia zawadi za pikipiki, televisheni, simu za kisasa na vyombo vya nyumbani.

Kwa mujibu wa Meneja Mkuu wa Global Publishers, Abdallah Mrisho, droo hiyo ndogo ni ishara ya kuanza rasmi kwa droo nyingi ndogondogo zitakazofanyika pia hadi mikoani, kuelekea droo kubwa ambayo itamtoa mshindi wa nyumba ya mamilioni ya shilingi iliyojengwa Dar.
Aliwataka wasomaji wa magazeti ya Global Publishers, ambayo ni Risasi, Championi, Uwazi, Amani, Ijumaa na Ijumaa Wikienda kuendelea kusoma na kujaza kuponi ili wajiweke katika nafasi nzuri ya kuibuka mshindi.

“Kuponi zote zitakazopokelewa zitashiriki katika droo zote, hata zile zitakazochezwa mikoani, kwa hiyo mtu anakuwa katika nafasi nzuri ya kupata ushindi endapo atakuwa na kuponi nyingi, ingawa siku zote bahati ni bahati, mshindi anaweza kushinda hata kwa kujaza kuponi moja tu,” alisema Mrisho.
PICHA: Richard Bukos | GLOBAL PUBLISHERS
Kwa stori zote kali, Tu-follow
Facebook @Globalpublishers
Twitter @GlobalHabari
Instagram @GlobalPublishers
YouTube @GlobalTVTZ