Vodacom Tanzania Foundation Na JKCI Washirikiana Kupanua Huduma Za Moyo Kwa Watoto

Afisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Vodacom Tanzania Plc Philip Besiimire akipeana mkono na Mkurugenzi Mtendaji wa Heart Team Africa Foundation (HTAF) Dkt. Naizihijwa Majani baada ya kusaini makubaliano ya ushirikiano yenye lengo la kuongeza nguvu kwenye mapambano dhidi ya magonjwa ya moyo kwa watoto hapa nchini kwa kuchangia asilimia 30 za gharama ya matibabu ambapo asilimia 70 zikiwa zimelipwa na serikali.


