The House of Favourite Newspapers
gunners X

Ziro Malaria Inaanza na Mimi, Nachukua Hatua Kuitokomeza

0

#ZIROMALARIA: Unaambiwa mbu anayeeneza Malaria hamuogopi baunsa wala mtu yeyote! Usipofuata maelekezo ya jinsi ya kujikinga na Malaria lazima utaambukizwa.

 

Ili kuwa salama, #Bi-Mdashi ambaye ndiye mhamasishaji wa jamii katika kupambana na ugonjwa wa Malaria, anakukumbusha kuchukua hatua zifuatazo kudhibiti Malaria.

 

– Lala ndani ya chandarua chenye dawa kila siku ili kujikinga dhidi ya mbu waenezao Malaria.

 

– Dhibiti mazalia ya mbu kwa kutunza mazingira.

 

– Nenda kapime kabla ya kutumia dawa za Malaria kwani siyo kila homa ni Malaria.

 

– Wahi kituo cha huduma za afya afya mara tu unapohisi dalili za Malaria upate tiba sahihi.

 

– Kamilisha dozi ya dawa mseto la Malaria kulingana na maelekezo ya mtoa huduma ili upone.

 

#ZiroMalaria Inaanza na Mimi, Nachukua hatua Kuitokomeza.

 

Tangazo hili linakujia kwa udhamini wa Wizara ya Afya chini ya Mpango wa Taifa wa Kudhibiti Malaria.

 

Leave A Reply