The House of Favourite Newspapers
gunners X

Benki Ya Exim Kuhudumia Sekta Kilimo cha Korosho

0
Meneja wa Benki ya Exim tawi la Mtwara, Ramadhani Magera akielezea kuhusu huduma mbali mbali za kilimo zinazotolewa na benki hiyo  mbele ya wadau wa zao korosho nchini wakati wa mkutano mkuu wa wadau hao  uliofanyika  mkoani Lindi hivi karibuni. Pamoja na mambo mengine Bw Magera alizungumza kuhusu namna hiyo iliyojakaunti ya MzalendoBenki hiyo ilikuwa moja ya wadhamini wakuu wa mkutano huo ambao pia ulihudhuriwa na Waziri wa Kilimo Bw Japhet Hasunga.

Benki ya Exim Tanzania mapema wiki hii ilishiriki kikamilifu kwenye mkutano mkuu wa wadau wa Korosho uliofanyika mkoani Lindi.

 

Pamoja na kuwa sehemu ya wadhamini wakubwa mkutano huo benki hiyo ilipata wasaa wa kuelezea fursa mbalimbali za kibiashara hususani katika zao hilo, mipango ya ukuaji na uboreshaji wa huduma inazotoa kwa wadau hao ikiwemo akaunti ya Mzalendo ambayo haina makato ya mwezi kwa wakulima hao.

Baadhi ya maofisa wa benki ya Exim wakielezea kuhusu huduma mbali mbali za kilimo zinazotolewa na benki hiyo  kwa mmoja wa wadau wa zao korosho alietembelea banda la benki hiyo wakati wa mkutano mkuu wa wadau hao  uliofanyika  mkoani Lindi hivi karibuni.

Akizungumza kwenye mkutano huo uliohudhuliwa na wadau mbalimbali wa zao la korosho wakiwemo wakulima, viongozi wa kiserikali, wafanyabiashara wakubwa na wadogo pamoja na wawakilishi wa vyama mbalimbali vya wakulima, Meneja wa Benki hiyo Tawi la Mtwara Bw Ramadhani Magera alisema benki hiyo imejipanga zaidi kutoa huduma zinazoendana na mahitaji ya wadau hao kwa wakati sahihi.

Ufuatiliaji wa Mkutano.

 

“Ukuaji wa benki ya Exim unaoshuhudiwa kwasasa ni matokeo ya ushirikiano baina yetu na wateja wetu wakiwemo wakulima ambao kwa kiasi kikubwa wameonyesha imani kubwa kwetu na hivyo kutuwezesha tuzidi kubuni huduma bora na rafiki za kibenki mahususi kwa ajili yenu ili kulinda na kurejesha imani mliyonayo kwetu,’’ alisema.         

Leave A Reply