The House of Favourite Newspapers

Henry Aanza Kuwapigisha Tizi Monaco

Thierry Henry.

THIERRY Henry juzi alianza mazoezi yake ya kwanza na Monaco, ikiwa ni siku chache tu baada ya kutangazwa kuwa kocha mkuu wa timu hiyo.

Gwiji huyo wa Arsenal, ambaye ni mchezaji wa zamani wa Monaco, amechukua nafasi ya Leonardo Jardim aliyetimuliwa klabuni hapo baada ya kikosi hicho kuwa katika hatari ya kushuka daraja.

 

Huku kukiwa na mchezo dhidi ya Strasbourg Jumamosi, Mfaransa huyo ililazimika haraka aanze mazoezi na kikosi hicho kinachosuasua msimu huu.

Henry pia alikwenda kwenye chumba cha kubadilishia nguo cha kikosi cha U-19 na kujitambulisha kwa wachezaji huku akisalimiana kwa kumshika mkono kila mmoja.

Comments are closed.