The House of Favourite Newspapers

MEYA AFUNGWA MIAKA TISA KWA KUFANYA NGONO NA MTOTO

Simon Thornton

MEYA wa zamani wa Godalming, Surrey, Uingereza, amehukumiwa kifungo cha miaka tisa jela kwa kufanya ngono na mtoto mdogo.

Thornton aliyekuwa meya kati ya mwaka 2006 na 2009 alikubali makosa 22 yakiwemo ya kufanya mapenzi na msichana alipokuwa na umri wa miaka 13 hadi 15.

Kesi hiyo ilifunguliwa mwaka huu na mwanamke huyo ambaye sasa ni mtu mzima.  Alifanya hivyo kutokana na ushauri wa wazazi wake na hasa baada ya kukutana na Thornton na kumwonyesha picha na filamu kadhaa alizozipiga wakati wakifanya naye ngono alipokuwa bado mdogo.

Kesi hiyo imewafanya polisi kutoa wito kwa waathirika wote wa ngono kuripoti polisi hata kama matukio hayo yalitokea miaka ya nyuma.

Former town mayor Simon Thornton arriving at Guildford Crown Court with his new partner before being jailed for nine years for child abuse 

Thornton akiwa na ‘mshikaji’ wake kabla ya kuhukumiwa kifungo cha miaka tisa kwa kumdhalilisha mtoto wa kike kingono. 

 

Comments are closed.