The House of Favourite Newspapers
gunners X

Mti wa Ajabu kwa ‘Babu Tale’, Unakusanya Kijiji Kizima – Video

0

MATULI ni kijiji kilichopo Ngerengere mkoani Morogoro, Jimbo la Morogoro Kusini-Mashariki chini ya Mbunge wake, Hamis Taletale (Babu Tale).

 

Kijiji hiki kina wakazi takribani 5,000 na miongoni mwa changamoto kubwa zinazokikabili  ni  miundombinu ya wawasiliano

 

Kijiji hiki kimegundulika mti mmoja ambapo  simu zote zinapatikana hapo,  hali iliyofanya wanakijiji hao kuupenda ili  kufanya mawasiliano ya simu na jamaa zao  walio nje ya kijiji hicho.

 

Ili mtandao ukamate, wanakijiji wanasema  mtu anahitajika kuweka simu yake kwenye moja ya makopo yaliyotundikwa hapo ili kupata mawimbi ya mitandao. 

 

Leave A Reply