Rais Samia Aongeza Kiwango cha Mkopo kwa Wanafunzi wa Elimu ya Juu – (Video+Picha)

Rais Samia Suluhu Hassan ametangaza kuongeza kiwango cha mkopo kwa wanafunzi wa elimu ya Juu maarufu kama ‘boom’ hadi kufikia shilingi 10,000 kwa siku.
Rais Samia amesema hayo Februari 11, 2023 wakati akizungumza na Wawakilishi wa Jumuiya ya Wanafunzi wa Taasisi za Elimu ya Juu Tanzania (TAHLISO) na Zanzibar (TAHLIFE), Ikulu Chamwino Dodoma.
Awali, wanafunzi wa vyuo vikuu waliopata mikopo, walikuwa wakipewa shilingi 8,500 kwa siku.
Rais Samia amewataka Watanzania hususan vijana, kutokubali kulazimishwa mambo ambayo ni kinyume na mila na tamaduni za Kitanzania.

